Ubeti wa kwanza (1 )
Kwa wanaonisikia , ni shairi si waraka
Naghani najifutua , pwamu zinanichemka
La mama najinyonyea , lengine sitotosheka
Kiswahili aminia , nyonyoyo naitosheka
Ubeti wa pili ( 2 )
Zengine mi huongea , ila sipendi hakika
Mama nimemzoea , nimeishi kuridhika
Manenoye asilia , matamu pita mipaka
Kiswahili aminia , nyonyoyo naitosheka
Ubeti wa tatu ( 3 )
Nini hicho mwatambia ,kama si lugha tukuka
Lugha yenye asilia , mashariki Afrika
Kenya na tanga twongea , burundi rwanda yafika
Kiswahili aminia, nyonyoyo naitosheka
Ubeti wa nne ( 4)
Mwacha chake mepotea , fasihiye ni fanaka
Methalize nazijua , misemo losemezeka
Na Vitendawili pia , na mafumbo ninashika
Nahau nazijulia , mbona nende kupotoka
Ubeti wa tano ( 5 )
Tamati nikijitua , nawaita kuitika
Mje nyote kuongea , lugha tamu na tajika
Asia weze enea , bara yote kadhalika
Kiswahili aminia , nyonyoyo naitosheka
Shairi hili limetungwa na mbilA
.
LikeLike
Bravo bro
LikeLike