Ubeti wa kwanza (1 )
Asali tamu ya guru , raha kutekerenyeka
Kupatiwa kwa uhuru, nafsi yanyong’onyeka
Hii haina ushuru , K.R.A yaumbuka
Mapenzi hasa Napewa , sikuiga ni kufana
Ubeti wa pili ( 2 )
jinsi alivyoumbika , mbila mi nala vinono
Kitabu nikiandika , kalamu haishi wino
Niruhusu kutamka , uzi mepata mshono
Mapenzi hasa napewa , sikuiga ni kufana
Ubeti wa tatu ( 3 )
Mwali kungwi wake nani , wote nimpelekee
Anayoyafanya honey, hataki nijichokee
Bembelezi kitandani , naimbiwa nipumbae
Mapenzi hasa napewa , si kuiga ni kufana
Ubeti wa nne ( 4 )
Sauti yake hayuni , nyororo si karipia
Akiwa yu ubavuni , taratibu aongea
Nahisi mbingu fulani , peponi nishaingia
Mapenzi hasa napewa , si kuiga ni kufana
Ubeti wa tano ( 5 )
Umbo limeniridhia , kama chupa ya fanta
Zote nyanja mekolea , kidari chapwetepweta
Guu la bia lakaa , nyuma rojo latokota
Mapenzi hasa napewa , si kuiga nikufana
Ubeti wa sita ( 6 )
Mapishi ayajulia , viungo navyoungia
Mwiko nalo sufuria , matumizi nasifia
Na hakuna kusalia , chakulache maridhia
Mapenzi hasa napewa , si kuiga nikufana
Ubeti wa saba ( 7 )
Ameninasa samaki , napumba nimesinyaa
Mwengine katu sitaki , tengani nimenasia
Kwaheri mlo wa kiki, nafunga zangu aua
Nenda pewa yangu haki , si kuiga ni kufana
Shairi limetungwa na mbilA
Malenga, kitabu tukipate wapi?
LikeLiked by 1 person